Tuesday, November 8, 2016

 BREAKING NEWS


Kiongozi mstaafu waserikali mwingine Afariki dunia
Huyu ni JOSEPH MUNGAI ambaye kwa taarifa za awali amepoteza maisha leo jion tareh 8 decembar 2016 katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa
P . K . A    JOSEPH MUNGAI  
chanzo TBC 


Anayemkataa Magufuli anawakumbatia mafisadi
Na Adelinus Banenwa 

“Siku za mwizi ni arobaini” haya ni maneno ya wahenga ambayo hayana  kipingamizi kwa hali ya sasa inayoendelea nchini Tanzania baada ya siku takribani therathini na tano tangu tumpate raisi mpya wa awamu ya tano ambaye aliapishwa November 5 mwaka huu na kukabidhiwa nchi kutoka kwa mtangulizi wake
Rais Dr John Pombe Joseph Magufuli anaendelea kuonekana wa tofauti kutokana na kasi yake ya utendaji japo walio wengi hawashtushwi na kasi yake hiyo kutokana na kujulikana vyema hata wakati akiwa waziri katika wizara mbalimbali kama vile wizara ya ardhi, uvuvi, pamoja na na wizara ya ujenzi
Anajulikana kuwa mtu mwenye misimamo isiyo teteleka, anaichukia rushwa, hana makundi kwenye chama chake, hawakumbatii mafisadi, haya yote yanamfanya aendelee kuwa maarufu na kuzidi kupendwa na watanzania waliokata taama na nchi yao kwa muda mrefu
Katika kampeini zake tangu alipoteuliwa na Chama Cha Mapinduzi CCM kupeperusha bendera ya chama hicho katika nafasi ya uraisi alikuja na kauli mbiu inayosema “hapa kazi tu” wengi wa wananchi walisema kauli hii inaakisi utendaji wake wa kazi  katika chakato wa kuomba lidhaa kwa wananchi wamchague ili awe rais wa awamu ya tano aliweza kutembea kwa barabara zaidi ya kirometa elfu arobaini huku akisisitiza kuwa mabadiriko yanawezekana ndani ya CCM
Uchaguzi uliyokuwa na ushindani usiyo  kuwa wa kawaida na ambao haukuwai kutokea katika historia ya Tanzania tangu ilidhie mfumo wa vyama vingi 1992 na uchaguzi wa kwanza mwaka 1995kwa kuwa hadi siku ya kupiga kura hakujulikana nani atashinda licha ya kuwa “mwamba ngoma uvutia kwake” pengine kutokana na umaarufu wa wagombea hasa kutoka vyama vikuu nchini Chama Cha Mapinduzi CCM kikiwakirishwa na Magufuli na  Chama cha Demokrasia na Maendelea CHADEMA kikiwakilishwa na Edward Lowassa
Tarehe 29 october mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Tanzania jaji mstaafu Damiani Lubuva alimtangaza mgombea kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM John Magufuli kuwa mshindi wa kiti cha urais kwa asilimia 58.46% na kuaapishwa tarehe 5 november  kwa kutekeleza kauli yake ya hapa kazi tu rais Magufuli alianza kazi siku ya pili yake baada ya kuapishwa yaani tarehe 6 kwa kufanya ziara ya kushtukiza wizara ya fedha na kukuta takribani wafanyakazi sita hawapo ofisini wakati ni muda wa kazi
Magufuli hakuishia hapo alifanya ziara nyingine ya kushtukiza  hospitari ya rufaa ya Muhimbili na kukuta hali mbaya kwa wagonjwa pamoja na vifaa tiba huku mashine city scan zikiwa  hazifanyi kazi kwa zaidi ya mwezi mmoja.  maamuzi  ya kuvunja bodi ya muimbili na kumsimamisha kazi mkurugenzi wa hospitali hiyo ilikuwa hatua ya mwanzo katika kuhakikisha utekelezaji wa kauli mbiu yake na kutoa wiki mbili mashine hizo ziwe zinafanya kazi
Ziara za kushtukiza kwa kiongozi huyo hazikuishia hapo,baada ya hapo aliamia bandari na kuibua wizi uliokuwa ukiendelea bandarini hapo ikiwa ni pamoja na upotevu wa makontena, ukwepaji wa kulipa kodi uliokuwa ukifanywa na wafanywa na biashara wakubwa jambo lilimpelekea Rais kumsimamisha kazi mkurugenzi wa  bandari kabla ya kuvunja bodi ya bandari hiyona kulitaka jeshi la polisi kuwashikilia watuhumiwa wote kwa ajili ya uchunguzi.
Hatua ya kupunguza matumizi ya serikali na kuelekeza nguvu zake katika kuinua uchumi wa taifa Rais Magufuli ameamua kufutilia mbali baadhi ya sherehe zilizokuwa zimezoeleka kuadhimishwa kwa shamra shamra ndermo na vifijo kama sikukuu ya uhuru , siku ya ukimwi na badala yake fedha hizo zitumike katika kununulia madawa pamoja na vitanda vya hospitali ya rufaa ya Muhimbili na kupanga siku hizo kufanyika usafi wa mazingira nchi nzima “hatuwezi kuadhimisha miaka 54 ya uhuru huku watu wanakufa kwa kipindupindu” alisema Rais Magufuli
Mpaka sasa Rais Magufuli anaendesha nchi akiwa na Waziri mkuu Kassim Majaliwa ambaye pia kasi yake ya utendaji imeonekana kuwa sambamba na Magufuli mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika shirika la reli Tanzania na Zambia (TAZARA) na kugundua madudu ya ubadhirifu wa fedha uliokuwa ukiendelea katika shirika hilo
“Anayemkataa Magufuli anawakumbatia mafisadi” alisema kiongozi wa chama cha ACT Wazarendo Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni mbunge wa Kigoma mjini kupitia chama hicho alitoa kauli hiyo mnamo November 22 mwaka huu huku akiwataka wananchi kumuunga mkono katika kupambana na ufisadi uliokithiri hapa nchini hasa katika sekta za umma
“Nilipokuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge nilikuwa nikitoa taarifa mbalimbali zinazohusu wizi na uporaji uliofanywa katika ubinafsishwaji, sasa tumepata Rais anayetaka kupambana na ufisadi na kurudisha viwanda hivyo tunapaswa kumuunga mkono”alisema Zitto
Rais Magufuli amevunja rekodi ya watangulizi wake kwa kuendesha nchi zaidi ya siku 30 bila kuwa na baraza la Mawaziri ambapo anafanya kazi na Waziri mkuu pamoja na Makatibu wakuu wa wizara  husika huku utendaji ukionekana kuwa wa kasi ya ajabu licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa zikiwemo za kuwamaliza mafisadi na wala rushwa katika ofisi zote za umma na kudhibiti mianya waliokuwa wakitumia.
Kama alivyofanikiwa kudhibiti safari za nje kwa viongozi na kuzuia viongozi hao kutotumia viti vya daraja la kwanza ndani ya ndege,na kuzuia manunuzi ya magari mapya ya serikali kwa lengo la kupunguza matumizi ya serikali na kuongeza pato la Taifa.
Utendaji kazi wa Magufuli umesababisha mgogoro mkubwa wa Afrika Mashariki ambapo wananchi kutoka Kenya wamemtaka Rais wao Uhuru Kenyata aige mfano wa Rais wa Tanzania katika kuibua na kudhibiti ufisadi uliokithiri nchini Kenya, vivyo hivyo hata nchini Uganda.
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari mapema wiki hii ametakiwa na wananchi wake kuiga mfano wa Rais Magufuli katika kuongoza nchi na kudhibiti rushwa pamoja na mfumuko wa bei nchini Nigeria wakati wakizungumza na shirika la utangazaji BBC
Kauli ya Zitto kuwa anayemkataa Magufuli anawakumbatia mafisadi haina kipingamizi kwani mambo yaliyoshindikana kwa miaka mingi yameweza kufanikishwa ndani ya muda mfupi, ni vyema wananchi wakampa ushirikiano katika safari hii aliyoianzisha



Suleiman Bungara

Mbunge wa kilwa kusini SULEIMAN BUNGARA   (Bwege)