Saturday, October 17, 2015

Hivi ndivyo helikopta ilivyomuua shujaa Filikunjombe

chopa 2
Chopa (helikopta) aliyokuwa akitumia Mbunge wa jimbo la ludewa, Mhe. Deo Filikunjombe.
AJALI ya chopa (helikopta) iliyotokea usiku wa kuamkia jana, Oktoba 16, 2015 katika Hifadhi ya Selous, eneo la Msolwa mkoani Morogoro, imeyakatisha maisha ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo la ludewa, Mhe. Deo Filikunjombe (43), pamoja na watu wengine watatu waliokuwa ndani ya helikopta hiyo,
Deo-Filikunjombe
Deo Filikunjombe.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja, Mhe. Filikunjombe aliyekuwa akitetea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alikuwa na watu wengine watatu kwenye helikopta hiyo, akiwemo rubani, Kepteni William Silaa ambaye ni baba wa Jerry Silaa, Vitalis Blanka Haule anayetajwa kuwa ndugu wa Filikunjombe na Egdi Mkwera, Ofisa Tawala wa Mkoa wa Tarime na mtaalam wa mifugo.
Chopa
Polisi na wananchi wakiwa eneo la tukio  baada ya Chopa kuteketea kwa moto.
Chagonja alieleza kuwa helikopta hiyo yenye namba za usajili, 5Y-DKK ilikuwa ikitokea jijini Dar es Salaam kuelekea kusini huku taarifa nyingine zikieleza kuwa ilikuwa ikielekea jimboni kwake, Ludewa kabla ya kupata hitilafu ya injini ikiwa angani, baadaye ikaanguka na kulipuka, ikisababisha eneo lote la ajali kugubikwa na vumbi na moshi mzito.
chopaDeo Filikunjombe akiwa kwenye helkopta anayodaiwa kupata nayo ajali.
Habari zisizo rasmi zilizolifikia gazeti hili, zilieleza kuwa helikopta hiyo iliondoka jijini Dar es Salaam majira ya saa 9 alasiri. Kabla ya kuruka angani, vyanzo vyetu vinaeleza kuwa helikopta hiyo ilipata hitilafu ndogo za kiufundi ambazo hata hivyo zilirekebishwa na safari ikaanza bila matatizo.
“Ilipofika kwenye Hifadhi ya Selous, rubani aligundua kwamba kuna hitilafu kwenye injini, akawa anajaribu kutafuta sehemu ya kutua kwa dharura ndani ya hifadhi hiyo lakini kabla hilo halijatimia, helikopta ilipoteza mwelekeo kabla ya kudondoka na hatimaye kulipuka,” kilieleza chanzo chetu kwa sharti la kutotajwa jina gazetini.
12107262_10203566066031418_6703966378237878945_n (1)
…Wakiendelea kufanya uchunguzi eneo la tukio.
Habari nyingine zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii, zinaeleza kuwa helikopta hiyo ilianza kuwaka moto ikiwa angani kabla ya kuanguka kandokando ya Mto Ruaha unaopita ndani ya hifadhi hiyo ambapo baadhi ya maoni yalidai huwenda chopa hiyo ilihujumiwa na hivyo kutaka uchunguzi zaidi.

Msiba nyumbani kwa Filikunjombe, Mbagala Kijichi-Dar

Deo-FilikunjombeAliyekuwa Mbunge wa Ludewa kwa tiketi ya CCM, Deogratias Filikunjombe, enzi za uhai wake.filikunjombe (2) Mke wa marehemu Deogratias Filikunjombe, Sarah Filikunjombe (kushoto) akilia kwa uchungu baada ya kupata tarifa za kifo cha mumewe.filikunjombeNdugu, jamaa na marafiki wakionekana wenye huzuni nyumbani kwa Deogratias Filikunjombe.filikunjombe (3)Nyumbani kwa Deogratias Filikunjombe Mbagala Kijichi, Dar es Salaam.silaaCapt. William Silaa enzi za uhai wake.chopaFilikunjombe akiwaaga wananchi wake.
chopa 2Chopa iliyosababsha kifo cha Filikunjombe, Capt. William Silaa na watu wengine wawili.
Mbunge wa Ludewa Mhe. Deogratias Haule Filikunjombe amefariki dunia katia ajali ya Chopa katika hifadhi ya wanyama ya Selous, pamoja na rubani Kepteni William Silaa mfanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa.
Wengine waliofariki kwenye ajali hiyo ni Vitalis Blanka haule na Ofisa Tawala wa Wilaya ya Tarime, Bw. Egdi Mkwera ambaye alikuwa mtaalam wa mifugo.