NA K-VIS MEDIA
CELINA
Ompeshi Kombani, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Utumishi), amefariki dunia
akiwa kwenye matibabu nchini India. Kwa mujibu wa Naibu Spika wa Bunge Job
Ndugai, Marehemu Kombani alipelekwa nchini India mwezi mmoja uliopita
akisumbuliwa na malaria iliyoambatana na homa kali.
Kwa
mjujibu wa Ndugai, Mh. Kombani ambaye mara ya mwisho alikuwa mbunge wa jimbo la
Ulanga Mashariki, amefariki jioni hii ya Septemba 24, 2015 na mwili wake
utawasili jijini Dar es Salaam, Jumamosi Septemba 26, 2015.
Mh.
Kombani aliyezaliwa 19 June 1959,
alipata
elimu yake ya msingi Kwiro kuanzia mwaka 1968 hadi 1975, na baadaye kujiunga na
shule ya sekondari Kilakala mwaka 1975 hadi 1978. Mnamo mwaka 1979 alijiunga na
shule ya sekondari ya wasichana ya Tabora, (Tabora Girls), na kuhitimu mwaka
1981.
Mwaka 1982, Mh. Kombani alijiunga na Chuo cha IDM Mzumbe na kujipatia shahada ya Utawala wa Umma (B.A in Public Administration mnamo mwaka 1982 hadi 1985. Mwaka 1994 hadi mwaka 1995 Mh. Kombani alichukua shahada ya pili ya Utawala wa Umma, chuo Kikuu ch Mzumbe
No comments:
Post a Comment